Guguye, mabocho au mashinda-dovu ni spishi za samaki washawishi wa baharini wa familia Lophiidae katika oda Lophiiformes wanaopatikana katika Bahari ya Aktiki, ya Atlantiki, ya Hindi na ya Pasifiki. Samaki hawa wanaishi kwenye mchanga au matope ya matako ya bara na miteremko ya matako hayo kwa kina cha m 40 hadi karibu na m 2,000.
Kama wengi wa samaki washawishi wengine wana kichwa kipana sana na kinywa kikubwa kinachobeba meno marefu na makali yaliyopindika nyuma. Pia kama vile samaki washawishi wengine mwiba wa kwanza wa pezimgongo umebadilishwa katika kifaa cha uvuvi kwa mshipi (ilisio, Kiing. illicium) kinachobeba chambo cha umbo wa kibonge chenye nyama (eska, Kiing. esca). Kifaa cha uvuvi kiko kwenye ncha ya pua juu ya kinywa na hutumika ili kuvutia mawindo. Mabocho pia wana miiba miwili au mitatu ya pezimgongo iliyopo nyuma zaidi kichwani na pezimgongo tofauti lenye miiba mmoja hadi mitatu lililopo nyuma zaidi kwenye mwili mbele ya pezi-shahabu. Katika jenasi za asili za mabocho (Sladenia na Lophiodes), miingilio ya matamvua huendelea hadi mbele ya misingi iliyorefuka ya mapeziubavu. Katika jenasi zilizogeuka (Lophiomus na Lophius), na katika samaki washawishi wengine wote, miingilio ya matamvua haiendelei hadi mbele ya misingi ya mapeziubavu. Mabocho wakubwa kabisa huweza kuzidi urefu wa m 1.5.
Spishi kubwa kadhaa za jenasi Lophius, ambazo hujulikana kama "monkfishes" kaskazini mwa Ulaya, ni spishi muhimu zinazovuliwa kibiashara. Ini ya “monkfish”, inayojulikana kama "ankimo", inachukuka kuwa chakula kitamu sana nchini Japani.
Guguye, mabocho au mashinda-dovu ni spishi za samaki washawishi wa baharini wa familia Lophiidae katika oda Lophiiformes wanaopatikana katika Bahari ya Aktiki, ya Atlantiki, ya Hindi na ya Pasifiki. Samaki hawa wanaishi kwenye mchanga au matope ya matako ya bara na miteremko ya matako hayo kwa kina cha m 40 hadi karibu na m 2,000.
Kama wengi wa samaki washawishi wengine wana kichwa kipana sana na kinywa kikubwa kinachobeba meno marefu na makali yaliyopindika nyuma. Pia kama vile samaki washawishi wengine mwiba wa kwanza wa pezimgongo umebadilishwa katika kifaa cha uvuvi kwa mshipi (ilisio, Kiing. illicium) kinachobeba chambo cha umbo wa kibonge chenye nyama (eska, Kiing. esca). Kifaa cha uvuvi kiko kwenye ncha ya pua juu ya kinywa na hutumika ili kuvutia mawindo. Mabocho pia wana miiba miwili au mitatu ya pezimgongo iliyopo nyuma zaidi kichwani na pezimgongo tofauti lenye miiba mmoja hadi mitatu lililopo nyuma zaidi kwenye mwili mbele ya pezi-shahabu. Katika jenasi za asili za mabocho (Sladenia na Lophiodes), miingilio ya matamvua huendelea hadi mbele ya misingi iliyorefuka ya mapeziubavu. Katika jenasi zilizogeuka (Lophiomus na Lophius), na katika samaki washawishi wengine wote, miingilio ya matamvua haiendelei hadi mbele ya misingi ya mapeziubavu. Mabocho wakubwa kabisa huweza kuzidi urefu wa m 1.5.
Spishi kubwa kadhaa za jenasi Lophius, ambazo hujulikana kama "monkfishes" kaskazini mwa Ulaya, ni spishi muhimu zinazovuliwa kibiashara. Ini ya “monkfish”, inayojulikana kama "ankimo", inachukuka kuwa chakula kitamu sana nchini Japani.