dcsimg

Kolokolo ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Kolokolo ni ndege wadogo wa jenasi mbalimbali katika familia Cisticolidae. Wanafana na videnenda lakini mkia wao ni mrefu zaidi na wana rangi kali zaidi: kahawia, kijivu au kijani mgongoni na nyeupe, njano na/au nyekundu chini na pengine kichwani na mbawani. Spishi nyingi zina mkufu mweusi kidarini. Wanatokea Afrika kusini kwa Sahara katika misitu na mapori. Hula wadudu. Hulijenga tago lenye kuba ya manyasi, majani na/au vigoga katika kichaka. Jike huyataga mayai 3-5.

Spishi

Picha

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri

Kolokolo: Brief Summary ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Kolokolo ni ndege wadogo wa jenasi mbalimbali katika familia Cisticolidae. Wanafana na videnenda lakini mkia wao ni mrefu zaidi na wana rangi kali zaidi: kahawia, kijivu au kijani mgongoni na nyeupe, njano na/au nyekundu chini na pengine kichwani na mbawani. Spishi nyingi zina mkufu mweusi kidarini. Wanatokea Afrika kusini kwa Sahara katika misitu na mapori. Hula wadudu. Hulijenga tago lenye kuba ya manyasi, majani na/au vigoga katika kichaka. Jike huyataga mayai 3-5.

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri