dcsimg

Keremkerem ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Keremkerem ni ndege wa familia ya Meropidae. Wana rangi maridadi na mwili wao ni mwembamba. Domo lao ni refu na jembamba na mkia wa aina nyingi ya keremkerem una mileli mirefu katikati.

Ndege hawa wanaishi uwandani kwa kanda ya tropiki na nusu-tropiki ya Afrika, Ulaya na Asia. Hula wadudu, na nyuki, manyigu na mabunzi hasa, ambao wanakamatwa hewani. Kabla ya kula, ndege anatoa mshale wa mdudu akimgongia tawi la mti au kitu kigumu kingine.

Keremkerem hupenda kuwa pamoja kwa makundi. Huchimba mashimo ndani ya kando za mchanga kwa kutaga mayai yao meupe.

Familia ya Meropidae imegawika nusufamilia mbili: Nyctyornithinae (keremkerem wenye ndevu) na Meropinae (keremkerem wa kawaida).

Spishi za Afrika

Spishi za Asia

Picha

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri

Keremkerem: Brief Summary ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Keremkerem ni ndege wa familia ya Meropidae. Wana rangi maridadi na mwili wao ni mwembamba. Domo lao ni refu na jembamba na mkia wa aina nyingi ya keremkerem una mileli mirefu katikati.

Ndege hawa wanaishi uwandani kwa kanda ya tropiki na nusu-tropiki ya Afrika, Ulaya na Asia. Hula wadudu, na nyuki, manyigu na mabunzi hasa, ambao wanakamatwa hewani. Kabla ya kula, ndege anatoa mshale wa mdudu akimgongia tawi la mti au kitu kigumu kingine.

Keremkerem hupenda kuwa pamoja kwa makundi. Huchimba mashimo ndani ya kando za mchanga kwa kutaga mayai yao meupe.

Familia ya Meropidae imegawika nusufamilia mbili: Nyctyornithinae (keremkerem wenye ndevu) na Meropinae (keremkerem wa kawaida).

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri