Wadudu mabawa-vigamba ni wadudu wadogo hadi wakubwa wa oda Lepidoptera katika nusungeli Pterygota (wenye mabawa). Jina ni tafsiri ya jina la kisayansi. Wadudu hawa wanajulikana kama vipepeo na nondo.
Wadudu hawa wana mabawa kama viwambo, isipokuwa spishi kadhaa ambazo zina mabawa yaliyopunguka au hazina mabawa kabisa. Kinyume na wadudu mabawa-viwambo kwa kawaida mabawa yao yamefunikwa kwa vigamba ambavyo kweli ni manyoya yaliyofanyika kuwa bapa. Lakini mabawa ya spishi kadhaa yana sehemu bila vigamba zilizo nyangavu kwa hivyo (k.m. Nondo mkia-mshale mwangavu).
Sehemu za kinywa za spishi nyingi zimetoholewa kuwa mrija mrefu sana unaoitwa ulimi au proboski. Mrija huo hutumiwa kufyonza mbochi au viowevu vingine. Lakini spishi za Zeugloptera bado zina sehemu za kutafuna kama ndugu wao wa oda Trichoptera (Wadudu mabawa-manyoya).
Wachanga wa vipepeo na nondo huitwa viwavi. Hawafanani na wapevu kwa sababu hawana mabawa, wana sehemu za kinywa za kutafuna na wana miguu bandia kwenye fumbatio licha ya miguu sita ya kweli kwenye toraksi. Kwa kawaida viwavi hula majani ya mimea na mara nyingi shina pia na pengine hata matunda. Spishi fulani za viwavi hula wadudu wengine na nyingine ni vidusia.
Wadudu mabawa-vigamba ni wadudu wadogo hadi wakubwa wa oda Lepidoptera katika nusungeli Pterygota (wenye mabawa). Jina ni tafsiri ya jina la kisayansi. Wadudu hawa wanajulikana kama vipepeo na nondo.
Wadudu hawa wana mabawa kama viwambo, isipokuwa spishi kadhaa ambazo zina mabawa yaliyopunguka au hazina mabawa kabisa. Kinyume na wadudu mabawa-viwambo kwa kawaida mabawa yao yamefunikwa kwa vigamba ambavyo kweli ni manyoya yaliyofanyika kuwa bapa. Lakini mabawa ya spishi kadhaa yana sehemu bila vigamba zilizo nyangavu kwa hivyo (k.m. Nondo mkia-mshale mwangavu).
Sehemu za kinywa za spishi nyingi zimetoholewa kuwa mrija mrefu sana unaoitwa ulimi au proboski. Mrija huo hutumiwa kufyonza mbochi au viowevu vingine. Lakini spishi za Zeugloptera bado zina sehemu za kutafuna kama ndugu wao wa oda Trichoptera (Wadudu mabawa-manyoya).
Wachanga wa vipepeo na nondo huitwa viwavi. Hawafanani na wapevu kwa sababu hawana mabawa, wana sehemu za kinywa za kutafuna na wana miguu bandia kwenye fumbatio licha ya miguu sita ya kweli kwenye toraksi. Kwa kawaida viwavi hula majani ya mimea na mara nyingi shina pia na pengine hata matunda. Spishi fulani za viwavi hula wadudu wengine na nyingine ni vidusia.